Aliyosema Yesu Juu Ya Hizo Amri Kumi

 


Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha, kijana mmoja mwanaume mwenye ari kubwa aliharakisha kwenda kwake na kumwuliza, "Mwalimu, nitende jambo gani jema ili nipate uzima wa mielel?" (Mathayo 19:16). Yesu aliweza kuona yule kijana alikuwa akipambana na tatizo la fedha, ndipo akamshauri kuachana na mali yake na ku"zishik(a) amri" (fungu la 17).
Yule kijana mwanaume alijaribu kuukwepa utambuzi wa tatizo lake alioufanya Kristo kwa kuuliza ni amri zipi alizokuwa akiziongelea. Yesu akaorodhesha amri kadhaa katika zile Amri kumi (fungu la 18, 19).
Mwishowe, yule "mtawala kijana tajiri" aligeuka na kwenda zake kwa huzuni (mafungu ya 20-22). Kiakili yeye alizikubali zile Amri kumi, ila hakuweza kuitii roho ya ile Sheria kwa kuachana na njia yake ya maisha ya uchoyo.
Amri kumi zinatuonyesha sisi mipaka ambayo ndani yake unaweza kukua uhusiano wenye afya pamoja na Mungu na kila mmoja wetu. Yesu alisonda kidole chake kwenye utii kuwa huo ndiyo njia ya kuipata furaha ya kweli.
"MKIZISHIKA AMRI ZANGU, mtakaa katika pendo langu, kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. Mimi NIMEWAAMBIA NINYI ILI furaha yangu iwe ndani yenu, na FURAHA YENU IWE KAMILI." Yohana 15:10,11.

Comments

Popular posts from this blog

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

Ufanye Nini Unapoumizwa Moyo Na Watu Wako Wa Karibu/ Jinsi Ya Kupokea Uponyaji kwa Moyo Ulioumizwa