VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2
Mithali 4;23 " Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima” Karibu tuendelee kujifunza jinsi ya Kulinda Moyo, leo tunaendelea kwa Kuangalia Vinywa vya Moyo ambavyo kwa hivyo Moyo wa mtu Hula. Vinywa vya Moyo 1. Macho. Macho ni mdomo wa moyo, chochote kiingiacho kwa macho hicho huenda moja kwa moja kwenye moyo na hicho ndicho kiwezacho kuutia moyo Unajisi.Mtu anapokuwa anatazama kwa macho yake anakuwa anakula, yaani anamlisha mtu wa ndani (moyo wake).Yesu alisema mtu mwema kutoka kwenye akiba njema na mtu mwovu kutoka kwenye akiba mbovu, hapo juu nimekwambia kuwa Akiba hukaa ghalani na akiba haijii automatically kwenye ghala, bali huwekwa ghalani na ndipo baadae hutoka. Tuangalie kwenye Mithali Jinsi akiba inavyotengenezwa ndani ya moyo na baadae itadhihirika.Weka ili moyoni kuwa kuna milango ambayo kwa hiyo kilichoko ...