Amri Kumi Ni Mwongozo Muhimu Sana Wa Agano Jipya

 

Katika Agano jipya, Yakobo alitoa ushuhuda wake huu:
"Maana yeyote anayeishika sheria yote, lakini anajikwaa katika neno moja tu ana hatia ya kuivunja yote. Kwa maana yeye aliyesema; "Usizini, pia alisema, "Usiue", Usipozini, lakini ukiua, umekuwa mvunja sheria. Semeni ninyi, na kutenda kama watu wale watakaohukumiwa kwa sheria inayowapa uhuru. "Yakobo 2:10-12.

Charles Spurgeon, Mhubiri Mkuu wa Kibaptisti wa karne iliyopita alitangaza akisema." Sheria ya Mungu ni Sheria ya Mbinguni - takatifu, ya Mungu, na kamilifu---- Hakuna amri yake hata moja iliyozidi kiasi; hakuna amri yake hata moja iliyopungua mno, lakini yenyewe haina kifani kiasi kwamba ukamilifu wake ni uthibitisho wa Uungu wake." John Wesley, mmojawapo wa Waasisi wa Kanisa la Methodisti, aliandika maneno haya juu ya tabia ya kudumu ya sheria hiyo. "Sheria hiyo ya Maadili iliyo katika hizo amri kumi…. Yeye (Kristo) hakuiondoa…. Kila kipengele cha Sheria hiyo ni lazima kiendelee kuwa na nguvu juu ya wanadamu wote na katika vizazi vyote…. Sermons, gombo la 1, kurasa 221,222.
Billy Graham, Mwinjilisti wa Kiinjili wa Ulimwengu mzima aliyeheshimiwa sana, anaziheshimu sana Amri kumi kiasi kwamba ameandika kitabu kizima juu ya umuhimu wa amri hizo kwa Mkristo.

Comments

Popular posts from this blog

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

Ufanye Nini Unapoumizwa Moyo Na Watu Wako Wa Karibu/ Jinsi Ya Kupokea Uponyaji kwa Moyo Ulioumizwa