Biblia Inasemaje Juu Ya Watoto

 

Watoto ni kipawa kitokacho kwa Mungu - Mwa. 33:5. Inasema Mwanzo 33:5Akainua macho yake, akawaona wanawake na watoto, Baada ya salamu  kupita baina yake na ndugu yake Yakobo, yeye akaona, na tazama nyuma ya wanawake wenye watoto, Yakobo na wake wawili na wake vijakazi wawili,   watoto aliokuwa nao ambao kufanya wanawake na watoto wale ni mali ya wakufuatao kwa Yakobo alikuwa alifanya bila kutaja wake zake na watoto, wakati alituma wajumbe wake na yeye huku akiwaacha nyuma ya makundi mengine, Mwa 32:5;
Watoto ni urithi wa Mungu - Zab. 127:3.
Watoto wana wa wana ndio taji ya wazee - Mit. 17:6.
Watoto hujijulisha kwa matendo yao - Mit. 20:11.
Madaraka ya Wazazi Kwa Watoto Wao:
Kuwafundisha watoto neno la Mungu kila Mara - Kum. 6:6-7.
Kuwafundisha watoto kumcha Mungu - Kum. 31:12-13.
Kuwafundisha watoto maandiko matakatifu toka utotoni mwao - 2 Tim. 3:15.
Kuwalea katika njia ipasayo nao hawataiacha hata wakiwa wazee - Mit. 22:6.
Watoto wanapaswa kuadhibiwa mara wafanyapo makosa - Mit. 13:24; 22:15; 23:13-14; 29:15-17; Ebr. 12:5-9.
Wazazi hawapaswi kuwachokoza watoto wao - Efe. 6:4; Kol. 3:21.
Wazazi Wanapaswa kuonyesha mfano mzuri kwa watoto wao ili watoto waige tabia yao - 2 Tim. 1:5.
Wazazi wanapaswa kuwatunza kwa kuwatimizia mahitaji yao - 1 Tim. 5:8.

Wazazi wana madaraka juu ya Watoto:
Watoto wafundishwe kummkumbuke Muumba wao - Mhubiri 12:1.
Watoto wafundishwe utakatifu ili wamche Bwana - Mit. 24:21.
Watoto wafundishwe kumtii Mungu - Kum. 30:2.
Watoto wawe na utii wa kuyasikiliza mafundisho ya wazazi wao - Mit. 1:8, 9.
Watoto  wanapaswa wawaheshimu wale waliowazaa - Efe. 6:2; Ebr. 12:9.
Watoto wanatakiwa wayashike maagizo ya wazazi - Mit. 6:20; Efe. 6:1; 3:20.
Watoto wanapaswa wawatunze wale waliowazaa - 1 Tim. 5:4.
Watoto wanapaswa wasifuate mfano mbaya wa wazazi wao - Ezekieli 20:18.

Watoto Waovu:
Watoto wa aina hii Huwadharau wazazi wao - Mit. 15:5, 20.
Watoto hawa Humlaani baba yao - Mit. 30:11.
Watoto Huwaaibisha wazazi wao - Mit. 19:26.
Watoto Ni msiba kwa wazazi wao - Mit. 19:13.
Watoto wa aina hii Huwahuzunisha wazazi - Mit. 17:25.
Watoto wa aina Huwadharau wazee wao - Ayubu 19:18.

Kwa Njia Nyingine Watoto Ni Mfano Kwa Watu Wazima:
Watu wazima wanapaswa kuupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo - Marko 10:15; Luka 18:17.
Ufalme wa Mungu ni wao - Marko 10:14; Mt. 19:13.
Wale wasiotubu na kuwa kama watoto wadogo hawatauingia ufalme wa Mungu hata kidogo - Mt. 18:3.
Wanapaswa kujinyenyekesha kama watoto wadogo - Mt. 18:4.
Katika uovu iweni watoto wachanga - 1 Kor. 14:20.

Watoto wa Wawakristo ni Watoto wa Mungu:
Watoto hawa Wamezaliwa mara ya pili kwa maji na kwa Roho - Yn. 3:3-5.
Watoto Wale wanaompokea Kristo ni watoto wa Mungu - Yn. 1:12.
Watoto hawa Ni watoto wa Mungu kwa njia ya imani - Gal. 3:23, 27.
Watoto Watendao haki ni watoto wa Mungu - 1 Yoh. 3:10.
Watoto Wale wanaoongozwa na Roho ni watoto wa Mungu - Rum. 8:14.
Roho hushuhudia pamoja na roho zao kwamba wao ni watoto wa Mungu - Rum. 8:16.
Watoto hawa Wanaitwa watoto wa Mungu na ndivyo walivyo - 1 Yoh. 3:1.
Watoto hawa ni watoto wa nuru - Yn. 12:36; Efe. 5:8; 1 The. 5:5.
Watoto hawa ni watoto wapendwao - Efe. 5:1.
Watoto hawa ni  watoto watiifu - 1 Pet. 1:14.
Watoto kama hao wao ni watoto wa ufufuo - Luka 20:36.
Lakini wengine huwa “watoto wa uasi” - Efe. 5:6; Kol. 3:6.
Watu wa aina hiyo watakuwa “wana wa laana” - 2 Pet. 2:14.
Watoto Huzaliwa Pasipo Dhambi (Hawana Dhambi). Angalia Dhambi

Comments

Popular posts from this blog

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

HAKI ZA WATOTO