HUDUMA YA PATAKATIFU

 



Miongoni mwa huduma ya lazima kwa wokovu wa wanadamu, lakini ambayo watu wengi, sana sana
hawaijui, ni hii ya Patakatifu. Yawezekana wewe u mmoja wao. Kwa hiyo, kabla hatujafika mwisho
wa masomo haya, napenda kukupa fursa hii ili upate kuifahamu huduma hii muhimu.
Katika kitabu cha Kutoka 25:8 tunasoma jinsi Mungu alivyomwambia Musa, “Nao na wanifanyie
Patakatifu ili nipate kukaa kati yao.” Hivyo kwa kuitikia agizo hili, mahali palijengwa yaani
Patakatifu au Hema ya kukutania au Hekalu (soma Kutoka 29:43-46, 40:1-11,7-38). Patakatifu
palikuwa na vyumba viwili kwa ndani, nje kulikuwa na madhabahu ya Sadaka ya kuteketezwa na
birika la kunawia makuhani, na ua uliovizingira vitu hivi vyote wa nguo ya kitani nzuri ya kusokotwa
(soma kutoka 38:9). Patakatifu au hema hii ilikuwa na chumba cha kwanza kilichoitwa “Patakatifu”
na chumba cha pili cha ndani kilichoitwa “Patakatifu pa Patakatifu”. Katika chumba hiki cha kwanza
cha “Patakatifu” kulikuwa na kinara cha taa, meza ya mikate ya wonyesho na madhabahu ya
kufukizia uvumba. Katika chumba cha pili yaani Patakatifu pa Patakatifu kulikuwa na Sanduku la
Agano na juu yake Kiti cha Rehema kikifunikwa na Makerubi. Kando ya sanduku kulikuwa na fimbo
ya Haruni iliyochipuka. Ndani ya Sanduku la Agano kulikuwa na mbao mbili zilizoandikwa amri
kumi za Mungu pamoja na mana. Vitu vyote hivi vilimwakilisha kristo na huduma yake ya
ukombozi. Mtu alipotenda dhambi, alikwenda na mnyama pale hemani kwa ajili ya huduma ya
upatanisho. Alipokuwa amefika kwa Kuhani (yaani mhudumu wa Patakatifu) pale madhabahuni (nje
ya hema) mdhambi aliweka mikono kichwani pa mnyama na kuungama dhambi zake. Baada ya
kuungama, yeye mwenyewe alimchinja mnyama yule na mnyama yule alitolewa pale madhabahuni
na kuteketezwa kuwa kafara kwa Bwana. Kwa imani dhambi ilihama toka kwa mdhambi na kuwa
juu ya mnyama aliyeuawa kwa ajili yake. Mtu huyu alirudi nyumbani akiwa huru. Lakini baadhi ya
damu ya mnyama ilichukuliwa na kuhani hadi chumba cha patakatifu na kunyunyizia katika pazia
lililotenga chumba cha patakatifu na kile cha Patakatifu pa Patakatifu, na kwa njia hiyo ile dhambi
ilipelekwa mbele za Mungu kwa ajili ya hukumu. Yaani dhambi ile lazima ipate kutengwa kabisa na
mtu aliyetubu. Pia kulikuwa na kafara maalum ya kutoa wanakondoo wawili mmoja asubuhi na
mmoja jioni. Huduma hizi zilifanyika kila siku isipokuwa siku moja tu kwa mwaka. Ndani ya hema
yaani katika chumba cha kwanza cha Patakatifu kulikuwa na huduma iliyofanyika kila siku, huduma
iliyokuwa ya kufukiza uvumba (soma Kutoka 29:38-42; Walawi 1:1-9, 4:1-12).
Mara moja kila mwaka, ilifanyika huduma iliyohusisha chumba cha pili cha hema yaani Patakatifu pa
Patakatifu. Huduma hii ilifanyika mara moja tu kwa mwaka ili kutakasa hema (Patakatifu) na watu
pia. Siku hiyo iliitwa siku ya upatanisho. Huduma hii ilifanywa na kuhani mkuu tu. Katika siku hiyo
kuhani alitoa ng’ombe kwa sadaka yake mwenyewe kufanya upanisho wa nafsi yake, ndipo afanye
huduma ya upatanisho kwa ajili ya watu. Huduma hii ndiyo iliyoondoa dhambi zote za wana wa
Israeli walizozitenda kwa mwaka mzima mbele za Bwana. Huduma hiyo ilihusisha mbuzi wawili –
mmoja kwa Bwana na wa pili wa Azazeli. Ni huduma ambayo kila mtu alipaswa kushiriki kwa njia
ya kujitaabisha roho yake (yaani kujihoji na kutubu dhambi yoyote aliyokuwa nayo ili apatanishwe na
Mungu). Kama mtu yeyote asingefanya hivyo, basi siku hiyo hiyo angekatiliwa mbali na watu wa
Mungu mara kuhani mkuu anapomaliza huduma ya siku ile (soma Walawi 16:1-34, 23:26-32,
Waebrania 9:1-10). Unaweza kujiuliza swali - kwani huduma hiyo inahusianaje na wokovu wetu?
Neno la Mungu linaonyesha kile kilichotokea siku ile Bwana Yesu alipokata roho pale msalabani -
“Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini----” (Mathayo 27:51).
Pazia hili ni lile lililokuwa linatenganisha vile vyumba viwili vya hekalu, yaani Patakatifu na
Patakatifu pa Patakatifu, na hii ilikuwa ishara kuwa huduma yote iliyofanyika hekaluni ili
kumpatanisha mdhambi ilikuwa imekoma hapa dunuani. Hakuna tena mwanadamu yeyote
anayeweza kufanya huduma hiyo na ikakubalika maana atakuwa anapingana na Mungu, na mtu
yeyote anayekwenda kwa kiongozi wa dini ili akaungame dhambi zake, pia atakuwa anapingana na
Mungu na huduma hiyo inakuwa ya bure tu (soma Mathayo 15:8-9). Sasa kama huduma ile ilikoma,
je mdhambi afanyeje sasa? Endelea kujifunza.
20
Biblia inasema, “---tunaye Kuhani Mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi
cha ukuu mbinguni, mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala
si mwanadamu. “-----watumikao mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni, kama Musa alivyoagizwa
na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema; maana asema, Angalia ukavifanye vitu vyote kwa
mfano ule ulioonyeshwa katika mlima” (Waebrania 8:1-5). “Basi ilikuwa sharti nakala za mambo
yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu
zilizo bora kuliko hizo” (Waebrania 9:23).
Ni wazi kuwa Patakatifu pa duniani na huduma zake ilikuwa ni nakala au mfano wa Patakatifu na
huduma za mbinguni. Sasa elewa nakala hizi kwa ukaribu au uwazi zaidi:
• Mnyama kwa sadaka ya kuteketezwa ya dhambi ilimwakilisha kristo kama kafara kwa
dhambi zetu (soma Yohana 1:29, Waebrania 9:13-14)
• Kuhani (mhudumu wa Patakatifu) alimwakilisha Yesu kama Kuhani wetu mkuu (soma
Waebrania 8:1-2, 4:14-15).
• Kinara cha taa kilimwakilisha Yesu kama nuru halisi (soma Yohana 1:9-14, 3:19, 9:5).
• Mikate ya wonyesho iliwakilisha jinsi mwanadamu anavyopata chakula chake kwa
Mungu (cha kimwili na cha Kiroho) kwanjia ya Kristo (soma Yohana 6:31-33).
• Madhabahu ya kufukizia uvumba iliwakilisha huduma ya Yesu ya kutuombea (soma
Waebrania 7:25, 1Yohana 2:1).
• Sanduku la agano (Amri Kumi) iliwakilisha tabia takatifu ya Mungu na kanuni pekee
ambazo wanadamu wanapaswa kuzitii. Utakatifu huo ndiyo “haki ya Kristo” (soma
Kutoka 19:5-6, Ezekieli 20:11-12).
• Kiti cha Rehema ni mahali ambapo utukufu wa Mungu (Shekina) ulionekana juu ya
lile Sanduku la Agano. Hii inaonyesha kuwa enzi yake Mungu wetu imejengwa katika
sheria zake ambazo ndio tabia yake (soma Lawi. 11:44, Zaburi 45:6-7). Ni mfano wa
kiti cha enzi cha mbinguni.
• Mbuzi wa Sadaka ya dhambi kwa ajili ya bwana (siku ya upatanisho) alimwakilisha
Kristo kama kafara ya Bwana kwa dhambi.
Mbuziw a Azazeli (siku ya upatinisho) alimwakilishNa i Skhuewtaan i. k uhani
mkuu alipokuwa amekwishamtoa ng’ombe wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya nafsi
yake na kufanya huduma zilizofuata, alikuwa akitoa pia mbuzi aliyekuwa sadaka ya
dhambi kwa ajili ya upatanisho wa Patakatifu, kwa sababu ya makosa ya Walsraeli,
na mambo yao machafu, na kwa ajili ya hema ya kukutania. Na baada ya huduma hii
ambayo ilihusisha kunyunyiza baadhi ya damu ya yule ngombe na mbuzi; juu ya kiti
cha rehema machafu yote ya wana wa Israeli yaliitoka madhabahu na Patakatifu
(hema) (soma Walawi 16:14-19). Baada ya huduma hiyo, alifanya huduma nyingine
kwa mbuzi wa pili (wa Azazeli), ambayo ilikuwa ni kuweka mikono yake juu ya
mbuzi huyo na kuungama uovu wote, makosa yote na dhambi zote za Israeli
(zilizotoka Patakatifu) juu ya mbuzi huyu, kisha alichukuliwa mbali jangwani na
kuachwa huko. Hivyo dhambi zote zilikuwa sasa zimetengwa mbali na mkutano wa
watu na Mungu (soma Walawi 16:20-28).
• Mnyama katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa iliwakilisha kafara ya Kristo
msalabani.
21
• Huduma ya kila siku iliyohusisha pia chumba cha kwanza cha Patakatifu ikiwakilisha
sehemu ya kwanza ya huduma ya Yesu katika Patakatifu pa mbinguni (soma Waebrania
7:26-28, 9:11-22).
Huduma ya siku ya upatanisho (siku ya Hukumu – soma Dan.7:9-10) iliwakilisha
huduma ya mwisho ya Yesu katika chumba cha Patakatifu pa Patakatifu mbinguni.
Huduma hii ndiyo inayoendelea sasa. Wote wanaomwamini Yesu na kutubu dhambi
zao watasamehewa na dhambi zao Yesu amezibeba, lakini atakapomaliza huduma hiyo,
dhambi zote zilizoungamwa zitawekwa juu ya Shetani (mbuzi wa Azazeli) aliye
mwanzilishi wa dhambi na ndiye atabeba hukumu ya dhambi hizo katika jehanamu.
Wale watakaokataa kumpa Yesu dhambi zao (kutubu) watapaswa kubeba hukumu au
mzigo wao wenyewe (soma Waebrania 9:23-28). Je, utachagua kundi gani?
Kwa hiyo sasa hivi hatuna haja ya kutoa wanyama kuwa kafara kwa dhambi maana Kristo tayari
amejitoa kwa ajili yetu. Hatuna haja kwenda kwa mtu yeyote ili kuungama mbele zake, bali
tunakwenda moja kwa moja kwa kuhani wetu wa mbinguni - Bwana Yesu - ili tuungame kwake.
Hakuna mwakilishi. Wakati wa Patakatifu pa duniani, mdhambi alikwenda yeye binafsi kwa kuhani.
Hakupitia kwa mtu mwingine ili amwombee, na hii ilikuwa nakala ya mambo ya mbinguni. Kwa
hiyo tumwendee Yesu moja kwa moja kwa njia ya maombi na kuungama dhambi zetu kwake, ili yeye
atuombee kwa Baba.
Jambo jingine muhimu ni kuwa ijapokuwa mdhambi aliondolewa dhambi alipopeleka mnyama wa
kafara, lakini ilimpasa kushirikiana na kuhani mkuu kwa huduma ya siku ya upatanisho na utakaso
kwa njia ya kujitaabisha roho yake, asije akakataliwa mbali na watu wa Mungu. Sasa wengi
wanaodai kumwamini Yesu kama mwokozi, wameishia tu pale katika huduma ya kafara katika
madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa (msalabani) na hawajui kuwa baada ya kutoa kafara, Kuhani
wetu mkuu - Yesu - ameingia Patakatifu pa mbinguni ili kukamilisha huduma yake ya Upatanisho -
ambayo ni kukomesha dhambi kabisa moyoni mwa muumini. Na kwa sababu hiyo, anasubiri kila
mtu atambue ukweli huu na kufanya uamuzi - halafu atatupa chini chetezo na kumaliza kazi ya
upatanisho na kupatakasa Patakatifu (soma Ufunuo 15:5-8). Mara tu Kristo atakapomaliza huduma
yake katika Patakatifu pa Patakatifu pa mbinguni, atakuja mara ya pili kwa wale wamtazamiao kwa
wokovu (soma Waebrania 9:28). Kwa hiyo, sasa hivi tuko katika siku kuu ya upatanisho. Kristo
yuko mbinguni mbele za Baba kwa ajili yetu. Huu ni wakati wetu kujitaabisha roho zetu kwa
kufanya toba kamili kwa Mungu wetu na kuwa na imani katika Kristo Yesu ili dhambi zetu
zisamehewe na kufutwa na Kristo awezekurudi na kutuchukua mbinguni. Kumbuka, mioyo yetu ni
hekalu ambalo Mungu anataka akae na kutawala. Je, tutamruhusu aingie na kutawala (soma Ufunuo
3:20-21)?
DHAMBI:
Katika masomo haya ambayo umeendelea kujifunza, naamini umeona wazi kuwa kilichosababisha
mpango huu wa wokovu ni dhambi. Nafasi hii tena ni ya kuiangalia dhambi kwa uwazi zaidi.
• Je, Dhambi ni nini? Neno la Mungu (Biblia) linasema “Kila atendaye dhambi afanya uasi,
kwa kuwa dhambi ni uasi” (1 Yohana 3:4).
• Uasi huu ni wa nini? Uasi huu ni wa torati au sheria ya Mungu (soma Warumi 7:7-8).
• Je, torati ina asili gani? “Ni takatifu, na ya haki na njema” na pia asili yake ni ya rohoni
(soma Warumi 7:12-14).
22
Unaposoma Warumi 7:15-24, neno la Mungu limeonyesha wazi hali yetu ya dhambi.
Imeelezwa kuwa imo ndani yetu na ndiyo sheria inayotawala viungo vyetu kiasi kwamba
hata tukitaka kutenda lililo jema, hatupati, maana hamna jema lolote ndani yetu isipokuwa
dhambi tu. Hii ni sawa na kusema nia ya miili yetu daima ni kutenda dhambi.
• Je maandiko yanasema nini kuhusu hii nia ya miili yetu? Warumi 8:6-7 inasema, “Kwa
kuwa nia ya mwili ni mauti, bali nia ya roho ni uzima na amani. Kwa kuwa ile nia ya
mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu. Wala haiwezi kuitii”.
Hali hii ya uadui juu ya Mungu ndiyo kila mwanadamu aliyo nayo. Ndiyo asili tunayorithi toka kwa
Adamu (soma Warumi 5:12, 3:10-18, Zaburi 14:2-3). Kumbuka lilitokea pale Edeni bustanini mara
Adamu na Hawa walipoasi walijikuta wamekuwa maadui wa Mungu na marafiki wa Shetani (soma
Yohana 8:44, 1 Yohana 3:8). Hivyo hakuna mtu yeyote anayeweza kukanusha kuwa kwa asili yake
hana uadui na Mungu. Si swala la uchaguzi ni la kurithi (soma 1 Petro 1:18). Kumbuka daima kuwa,
dhambi ni ile nia ya mwili ambayo ni uasi wa sheria za Mungu, ni uadui juu ya Mungu. Ndiyo maana
tunapaswa kutafakari upya juu ya maisha yetu na yote tuyawazayo, tusemayo na kuyatenda. Je, ni nia
ya miili (Nafsi) yetu au ni mapenzi ya Mungu. Na ili kujua kama ni mapenzi ya Mungu au la, njia ni
kuyapima kwa nuru ya neno la Mungu. Ikiwa ni sawa sawa na neno hilo, basi jambo hilo si dhambi
(soma Isaya 8:20).
Siku hizi yapo mambo mengi sana yanayofanyika kinyume kabisa na neno la Mungu, na tena
mengine kwa jina la dini, na watu wengi wanafikiri ni sawa tu. Wengine hujaribu kupima na kusema
dhambi hii ni ndogo tu na haiwezi kumzuia mtu kuingia mbinguni. Yote haya ni hila za Shetani
kuwadanganya wanadamu ili hatimaye wapotee. Usidanganyike mpendwa, Biblia inasema ,“Mungu
hadhihakiwi, kwa kuwa chochote apandacho mtu, ndicho atakachovuna, maana yeye apandaye kwa
mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu,; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho
atavuna uzima wa milele” (Wagalatia 6:7-8). Dhambi ndogo au moja ni nia ya mwili ambayo ni
uadui juu ya Mungu. Dhambi kiasi au nyingi ni nia ya mwili ambayo ni uadui juu ya Mungu. Hivyo
wote ni maadui wa Mungu na ndiyo maana hukumu yao ni moja tu - ziwa la moto. Yakobo 2:10.12
inasema, “Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa
juu ya yote. Maana yeye aliyesema usizini, pia alisema usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini
umeua, umekuwa mvunja sheria ----.” Jipime katika sheria takatifu (amri kumi) za Mungu ili ujue
uko kwa Mungu au kwa shetani aliye mwenye dhambi.
Kristo Yesu pekee ndiye tumaini letu la wokovu. Hebu tufungue mioyo yetu ili aingie na kutushindia
dhambi. Kumbuka torati au sheria ya Mungu asili yake ni ya rohoni.
Hivyo uasi wa sheria hii pia unaanzia moyoni (soma Isaya 14:13-14, Ezekieli 28:17). Uasi ulianzia
moyoni mwa Lusifa na akawa Shetani. Adamu na Hawa walitenda dhambi (kula tunda) wakati
walipopoteza uhusiano na Mungu mioyoni mwao. Hivyo kula tunda ilikuwa ishara ya nje ya uasi
moyoni. Badala ya kumwamini Mungu, walimwamini Shetani. Ndivyo ilivyo leo, wale wote
wanaomwamini Yesu, wanapewa uwezo kufanyika wana wa Mungu. Hili si swala la kinywani tu,
bali ni la moyoni pia (soma Warumi 10:9-10). Wale wanaomwasi Mungu na kumwamini Shetani
wanaendelea kutenda dhambi na mwisho ni kuangamia milele (soma Ufunuo 21:8).

Comments

Popular posts from this blog

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

Ufanye Nini Unapoumizwa Moyo Na Watu Wako Wa Karibu/ Jinsi Ya Kupokea Uponyaji kwa Moyo Ulioumizwa