Jinsi kutumia Muda Wako Vizuri

 

Wakolosai 4:5 Waefeso 5:14-16

Maana ya Muda

Muda ni mali yenye dhamani kama ilivyo pesa yako, nyumba yako, gari lako, kitanda chako nk

Ndio maana wazungu wanasema “Time is Money”

Sifa za Muda

  Hautengenezwi

Hautengenezwi na mtu, ni Mungu mwenyewe ametupa kwa hiyo ni busara kuutumia vizuri

Haufugiki

Haufugiki ukipotea umepotea, haurudi

“Opportunities comes and go, they will never come back”

“Fursa huja na kwenda, hazirudi tena”

Muda ni maisha

If you love life, don't waste time, for time is what life is made up of.   Bruce Lee

Hausubiri,

Wakati ni ukuta (ina mwisho)

“Time the time before it times you”

Lost time is never found again.   Benjamin Franklin

 

“Time is what we want most, but what we use worst.”   ― William Penn

 

“You may delay, but time will not.”
― Benjamin Franklin

Kwa nini kutumia muda vizuri?

Tunatumia muda vizuri kwa sababu nyakati hizi ni za uovu

Usipoutumia muda vizuri, utautumia vibaya kwa kufanya maovu -Waefeso 5:16

Faida za kutumia muda vizuri

a.       Kukua kiroho

b.      Kupata maendeleo ya kielimu, kiuchumi, nk

c.       Kuheshimika katika jamii

d.      Kutengeneza mahusiano mazuri na wenzako

Hasara za kutumia muda vibaya

e.      Kudumaa kiroho

f.        Kurudi nyuma kimaendeleo kama ya kielimu, kiuchumi, nk

g.       Kukosa heshima katika jamii

h.      Kuharibu mahusiano mazuri na wenzako

 

Hatua za Jinsi ya Kutumia Muda Wako Vizuri

1.     Kumtanguliza/Kumtegemea Yesu

Kumtanguliza/Kumtegemea Yesu Katika Muda/Ratiba Yako Waefeso 5:14

2.     Kutathmini jinsi ulivyotumia muda huko nyuma 

Kutafakari na kutathmini jinsi ulivyotumia muda huko nyuma  Waefeso – 5:15

a.       Weka ratiba yako ya zamani ikiwa na vitu/shughuli muhimu kama kazi zako za kawaida, shughuli za kiroho kama maombi, kuhubiri, kushuhudia nk, shughuli za kanisani

b.      Weka maksi kwa kukadiria ni shughuli ngapi umeweza kutimiza kwa ufanisi upi na zipi hukufanikiwa

c.       Eleza pia nguvu na fursa zilizokuwezesha kufanikiwa na udhaifu pamoja na pingamizi zilizosababisha ushindwe kutimiza

Mfano wa ratiba ya tadhimini

Tarehe

Kazi/Shughuli

Kiwango cha ufanisi ktk %

Sababu za ufanisi au za kushindwa

2.       Kubuni na kupanga ratiba kwa kuzingatia tathmini hapo juu Waefeso 5:16, Wakolasai

Mfano wa ratiba ya maboresho

Tarehe

Kazi/Shughuli

Kiwango cha ufanisi

3.     Kuweka vipaumbele

Kuweka vipaumbele katika kuitekeleza ratiba yako Waefeso 5:16, Wakolasai 4:5,

Jedwali la shughuli za kila siku



         

HARAKA

SIO HARAKA

MUHIMU

I - Matatizo

Msongo wa Matatizo

II  - Kazi za Maendeleo

Kufanya mambo katika mpangilio mzuri

SIO MUHIMU

III – Dharura

Kuendeshwa na mambo ya watu wengine

IV - Vipoteza Muda

Kufanya mambo yasiyo kwenye ratiba



Jedwali linaloonyesha aina ya shughuli na vipaumbele

HARAKA

SIO HARAKA

MUHIMU

I - Matatizo

Msongo wa Matatizo

§  Kifo, mafuriko, magonjwa n.k.

Kazi zote muhimu na haraka lakini ni nje ya ratiba.

Ratiba: Huongozwa na matatizo

Matokeo ni: Kukosa maendeleo ya kimwili na kiroho. Kwa sababu ya kufanya mambo kwa kiti moto, mahangaiko tu na kuchanganyikiwa

II  - Kazi za Maendeleo

Kufanya mambo katika mpangilio mzuri

§  Kujenga nyumba

§  Kulima shamba

§  Kusoma na kusomesha

§  Kuhudhururia ibada nk

Kazi zote ambazo sio za haraka lakini ni za kupangwa.

Ratiba: Huongozwa na mpangaji wa ratiba

Matokeo ni: Kupata maendeleo ya kimwili na kiroho kwa sababu ya Nidhamu na Mpango Mzuri wa kazi nk

SIO MUHIMU

III - Dharura

Kuendeshwa na mambo ya watu wengine Simu, barua, mgeni, harusi, mialiko n.k.

Kazi zote zinazoingilia ratiba ambazo sio muhimu lakini ni za haraka.

Ratiba: Huongozwa na watu wengine

Matokeo ni: Kukosa maendeleo kwa sababu ya Kupelekeshwa na wengine, kufanya kazi katika woga, hakuna kuona mbali hapa

IV - Vipoteza Muda

Kufanya mambo yasiyo kwenye ratiba

Karata, Bao, Kutembelea wengine,

Kuangalia TV, Radio, Video, Facebook, n.k.

Vitu vyote vya kupoteza muda

sio muhimu, sio haraka.

Ratiba: Hakuna ratiba kwa sababu ya ambo yasiyopangwa

Matokeo ni: Umaskini, kurudi nyuma kiroho, Kutowajibika kwa ujumla, kufukuzwa kazini, kuwa mzigo kwa ndugu au rafiki

Kumb: Asiyefanya kazi na asile 2Thel 3:10,11

 4.     Kuomba Hekima

Kuomba Hekima Katika Kusimami na Kutekeleza Ratiba na Mambo nje ya Ratiba (mambo ya dharura hasa yale ya kiboksi cha kwanza) Waefeso 1: 17, Yakobo 1.5

5.     Kutoahirisha jambo

Jizoeze kutoahirisha jambo/mambo/shughuli

6.     Kufanya mambo zaidi ya moja kwa wakati mmoja

Jizoeze kufanya mambo zaidi ya moja kwa wakati mmoja kwa yale mambo yanayowezekana

7.     Kuweka kumbumbuku ya namna ya kufanya jambo

Kuweka kumbumbuku ya namna ya kufanya jambo kwa urahisi na ufanisi zaidi ili ikusaidie kwenye utendaji wa huko mbeleni kwa kuboresha zaidi

Hitimisho

Katika kuhitimisha ni vizuri kujua na kuukubali ukweli kuwa matumizi ya muda ni ya tabia na utamaduni zaidi. Hivyo hauwezi kuwa jana tu unatumia muda vibaya na leo ukageuka na kuwa unatumia muda vizuri.

Ili uweze kubadili tabia na utamaduni wako wa kutumia muda vibaya kwenda kwenye maadili ya kutumia muda vizuri ni vyema yafuatayo yatokee kwako:

1.       Kukubali ukweli na kukubali kugeuka kwa kubadilika kifikra

2.       Kumtanguliza Mungu katika yote

3.       Kukubali pia kujifunza namna ya kuutumia muda vizuri kutoka katika maandiko na walimu au marafiki zako

4.       Kuchukua hatua ya kujizoeza kuutumia muda vizuri kwa kufanya kidogokidogo

5.       Kijitathmini kila baada ya muda Fulani (hapa unaweza kuwatumia watu wengine)

6.       Fundisha la elekeza haya kwa watoto wako

Mungu akubariki na kukuwezesha kuutumia muda vizuri

 

Comments

Popular posts from this blog

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

Ufanye Nini Unapoumizwa Moyo Na Watu Wako Wa Karibu/ Jinsi Ya Kupokea Uponyaji kwa Moyo Ulioumizwa