KRISTO AKIPOKELEWA MOYONI:
1. Atakupatanisha na Mungu kwa kuondoa ile nia ya mwili ambayo ni uadui juu ya Mungu. Nia ya
mwili ndiyo dhambi (soma Waefeso 2:13-17, 1 yohana 2:2, 3:8, 1Timotheo 2:5). TOBA!
2. Utasamehewa dhambi (soma Warumi 3:25-26, Mathayo 2:37-38, 3:19, 1 Yohana 1:8-9).
3. Anakupa uwezo kufanyika mwana wa Mungu, yaani uwezo wa kutii sheria za Mungu kikamilifu
(soma Yohana 1:12-13, 14:15, 15:1-8).
4. Anakupatia uzima wa milele (soma Yohana 3:16, 5:24-29, 6:39,48-58).
23
5. Anakupatia ushindi juu ya dhambi (soma 1 Kor. 15:57, Warumi 7:25, 1 yohana 5:3-5, Ufunuo
12:11).
Yote haya Mungu wetu ametupatia kutokana na upendo ulio mkuu kwetu wanadamu. Neno lake
linasema, “mmeokolewa kwa neema” (Waefeso 2:8-9). Neema hii imefunuliwa katika Kristo Yesu.
Na yeyote anayempokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake anakuwa ni adui wa Shetani
maana ndani yake kuna adui ya Shetani, na vita vile vilivyoanza mbinguni vinajitokeza kwa sura ya
juu zaidi. Lakini Bwana asifiwe, Kristo Yesu ameshinda.
Comments
Post a Comment