KUHESABIWA HAKI (HAKI KWA IMANI)
Haki ni nini? Ni kutenda haki (mema) au utakatifu. Je, mtu yeyote anaweza kuitenda iliyo haki? La,
hasha maana ndani yetu sisi, hakuna lililo jema (soma Warumi 7:14-19). Mti mbaya unawezaje kuzaa
matunda mazuri, (Mathayo 12:34)?
Nini maana ya kuhesabiwa? Kuhesabiwa ni kupewa kitu bila kukifanyia kazi au bila kustahili. Hivyo,
kuhesabiwa haki au utakatifu ni kupewa haki hiyo sisi tulio wadhambi. Yaani badala ya kuhesabiwa
kuwa wadhambi tunahesabiwa kuwa watakatifu. Je, jambo hili linawezekana kabla ya sisi kushika
amri za Mungu? Ndiyo na ndivyo ilivyo maana ndani yetu hakuna jema. Haki hii tunayopewa bure
ni ya nani? (soma Isaya 52:3). Isaya 45:24.25 inasema, “---- kwa Bwana peke yake, iko haki na
nguvu-----. Katika Bwana wazao wote wa Israeli watapewa haki, na kutukuka”. Tulitangulia kuona
kuwa Kristo ndiyo haki yetu. Sasa swali kubwa ni kuwa ni kwa jinsi gani haki (utakatifu) ya Kristo
unakuwa wetu? Neno la Mungu linasema ni pale tunapomwamini Yesu kama Bwana na mwokozi
wetu (soma Warumi 3:23-24). Ni wakati gani Mbingu zinapomhesabu mtu kuwa amemwamini
Yesu? Ni pale mtu anapoona utakatifu wa sheria ya Mungu kwa kuona na kutambua gharama
iliyolipwa msalabani; akaona na kutambua ubaya wa dhambi zake, akaichukia dhambi na kukusudia
kuicha kabisa moyoni, akatamani na kukubali kupokea kwa njia ya imani maisha matakatifu ya
Kristo. Hapo ndipo haki ya Kristo inapowekwa badala ya dhambi za mtu, na anahesabiwa kuwa
mtakatifu. Yaani, ni lazima tukubali kubadilishana na Bwana Yesu - sisi tumpe dhambi zetu zote, na
yeye anatupatia maisha yake matakatifu. Huku ndiko kutubu kwa kweli kutakakomfaa mdhambi. Je,
mwanadamu anaweza kulifanya hili yeye mwenyewe? La. Mungu pekee ndiye anayelianzisha ndani
ya mdhambi (soma Mathayo 5:30-31; 4:12, Waefeso 2:8-9). Kumbuka Mwanzo 3:15 na Waebrania
12:2-3. Ndipo tutakapoona upendo huu mkuu wa Mungu kwetu unatupatia amani na Mungu. Na ni
amani hii ya Kristo moyoni inaweza kutupatia furaha ya kumtii Mungu maishani. Mtu anapokuwa
amehesabiwa haki (amesamehewa dhambi) (soma Warumi 4:6-8), Mungu anafanya kitu kingine zaidi
kwa mtu huyo (soma Ezekieli 36:25-27, Yohana 3:7-8, 2 Kor. 5:17, Waebrania 8:10). Mtu anazaliwa
mara ya pili (upya) na anakuwa kiumbe kipya. Na mtu anapokuwa kiumbe kipya, ataishi maisha
mapya, siyo yale ya zamani. Maana si yeye atendaye, bali ni Kristo atendaye kazi ndani yake kwa
njia ya Roho Mtakatifu (soma Wagalatia 2:20, Yohana 15:1-5, Wafilipi 2:13, Warumi 6:17-18, 22).
Kwa hiyo mtu anaendelea kukaa katika utakaso, na Mungu mwenyewe akiwa ndiye mtendaji,
mwanadumu anadumu kuwa mpokeaji kwa njia ya imani, maana Mungu ndiye mwanzilishi na
mkamilishaji wa imani yetu (soma Waebrania 12:2). Hadi hapo bado mwanadumu hana la kujisifia,
maana matendo hayo si yake mwenyewe (soma Warumi 3:27), bali ni Roho wa Kristo aliye ndani
yake (soma Wagalatia 5:22-25).
Wengi wanaweza kufikiri kuwa tayari wamempokea Yesu kwa maana halisi inayoelezwa na
maandiko. Lakini unajua watu wa Mungu wa Kanisa la Mitume waliupindua Ulimwengu wa wakati
ule kwa injili ya milele? Je, kile kilichofanyika wakati ule, unakiona leo? Unajua kwa nini hali ile
ilikuwa tofauti na hii ya sasa? Hebu soma na kutafakari mafungu haya kwa makini. 2 Kor.5:14-15
inasema, “Maana, upendo wa Kristo watubidisha, maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja
alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote; tena alikufa kwa ajili ya wote; ili walio hai wasiwe hai
tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa akafufuka kwa ajili yao”.
Unakumbuka ile sheria kuu ya mbinguni? Ni Upendo usio na ubinafsi.
12
Kanisa la nyakati za mitume walipotambua upendo wa Mungu kwa ajili yao katika Kristo Yesu,
walijitoa, Walijisalimisha kwa Mungu, wao na vyote walivyokuwa navyo (soma Warumi 12:1).
Ndipo mbingu zikawamwagia roho Mtakatifu siku ya Pentekoste, ambayo matokeo yake yaliupindua
ulimwengu (soma Matendo 17:6). Waumini walipokuwa wakitoa nyumba zao, wakiuza viwanja na
vitu vingine wakavileta miguuni pa mitume, walikuwa wakionyesha upendo wa Yesu ndani yao
ulivyokuwa ukibubujika. Waliishi si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa
akafufuka kwa ajili yao, yaani Yesu.
Ubinafsi ulitoka. Wakajazwa upendo wa mbinguni usio na ubinafsi. WAKAISHI KWA AJILI YA
YESU. Je, unaweza kuthibitisha kuwa pale ulipoamini, ulijitoa kwa ajili ya hilo? Yaani ulijitoa kabisa
uishi kwa ajili ya Yesu tu, si kwa faida yako mwenyewe? Je tumekuwa tayari kiasi gani kutoa mali
zetu kwa ajili ya Yesu? Vipi kuhusu muda wetu – je, unatumika kwa ajili ya Yesu, iwe kwa
kuhudhuria vipindi mbalimbali vya ibada nyumbani, kanisani au mahali pengine? Vipi kuhusu siku
yake takatifu ya Sabato? Je, saa inapofika kati ya kumtukuza Bwana Yesu na nafsi yako, humsaliti
Yesu ukamwacha na kusema utarudiana naye baadaye ukiisha timiza matakwa ya nafsi yako? Kuishi
kwa ajili ya Yesu, ni kumruhusu daima katika mambo yote atimize kusudi lake jema ndani yako(soma
Warumi 8:28). Unajua mtu anaweza kuingia kanisani, akabatizwa, akatunza Sabato pamoja na amri
nyingine zote, akatoa zaka na sadaka, akahubiri injili na kufanya mambo mengine mengi, lakini,
msukumo wa kufanya yote haya ukawa ni ubinafsi. Mara nyingi watu wa jinsi hii huhesabu yale
waliyofanya na kujilinganisha na wengine, lakini hebu jipime na Yesu Kristo peke yake ndipo
utayaona mambo kwa nuru ya mbinguni - nuru halisi. Isaya 64:6 inasema, “Kwa maana sisi sote
tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa
unajisi, sisi sote twanyauka kama jani, na maovu yetu yatuondoa, kama upepo uondoavyo”. Yaani
mwanadamu anaweza kutenda matendo yanayoonekana kuwa ni ya haki lakini bado ni mwovu tu.
Dhambi imetuchafua kiasi kwamba pasipo damu ya yesu kamwe hatuwezi kuwa safi (soma
Waebrania 9:22). Dhambi imo ndani yetu na haiwezi kuondolewa kwa namna yoyote tunayoweza
kufanya (soma Warumi 7:7-10, 18). Sheria ya Mungu ya upendo, iletayo uzima, ndani yetu inaleta
mauti. Asili ya dhambi ndiyo tuliyorithi kwa baba yetu Adamu, na katika hali hiyo kamwe hatuwezi
kuwa wana wa Mungu, isipokuwa tunakubali kuingia na kuzaliwa kwa Adamu wa pili, yaani Kristo
(soma Warumi 5:17, 1 Korintho 15:45-49). Hebu fikiria, kama leo ungeamua kuacha matendo yote
maovu uliyokuwa unafanya na kuanza kutenda mema, je maovu yako yaliyopita ungeyaondoaje? Au
ukisema matendo yako mema ya sasa yatafidia yale maovu, je ungefuta kumbukumbu lake? Soma
Yeremia 2:22. Ni kwa kumpokea mwanakondoo wa Mungu tu, ndipo dhambi zetu zinaondolewa.
Kufanya vinginevyo ni sawa na kukiosha kikombe kwa nje na ndani kikabakia ni kichafu. Ni pale
kikombe kinapooshwa ndani, ndipo na nje huwa safi (soma Mathayo 23:25-26). Kutafuta kuhesabiwa
haki kwa matendo ya sheria ni unafiki na ndio maana ni machukizo kwa Bwana. Mtume Paulo
anasema, alipotambua kuwa hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa
matendo ya sheria, wao waliokuwa Wayahudi walimwamini Yesu (soma Wagalatia 2:15-16). Je,
Paulo alipomwamini Yesu hakuwa na dini au matendo mema? Hebu soma Wafilipi 3:4-7, anasema,
“Walakini mimi ningeweza kuutumaini mwili, mtu yeyote akijiona kuwa anayo sababu ya
kuutumainia mwili (yaani matendo) mimi zaidi. Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli,
wa kabila ya Benyamini, Mwebrainia wa Waebrainia, kwa habari ya kuishika torati, ni farisayo, kwa
habari ya juhudi, mwenye kuliudhi kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na
hatia. Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.”
Paulo anatuonyesha matendo yake mema ya kidini aliyokuwa nayo, na haya ndiyo aliona si kitu, ni
hasara tu. Fungu la 8 anasema, “Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili
ya uzuri usio na kiasi kwa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata
hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo”. Mpendwa! Unaweza
kuhesabu matendo yako mema yote uliyotenda nje ya Kristo (haki kwa imani), kuwa kama mavi?
Tafakari kwa makini sana jambo hili, je utakuwa tayari kuachana na haki yako binafsi?
Unajua, wanadamu wote kwa asili tunajaribu kutenda mema ili, kwanza, Mungu atupatie nafasi
mbinguni, tukayapate mema ya huko. Pili ni ili asije akatutupa motoni siku ya mwisho HUU NDIO
UBINAFSI UNAOSEMWA. Yaani tunaamini kwa kumpokea au kumkiri Yesu kule tunakofanya ni
kama kuingia shindano la bahati nasibu. Kwa hiyo Bwana Yesu ni kama tiketi ya kuingilia shindano,
halafu kila mmoja sasa akazane mwenyewe kuepuka jehenamu na kupata mbingu kwa matendo yake.
Ndiyo maana maneno kama “imani na matendo yako ndiyo yatakuokoa” husikika miongoni mwetu.
Lakini kumbuka ndani yetu hakuna lolote jema. Na kwa sababu kujipatia haki ya Mungu kwa bidii
13
zetu wenyewe haiwezekani, (lakini ndicho wanadamu tunachojaribu kufanya, maisha ya kutaka
kumfuata Yesu yamekuwa magumu na mzigo kwetu, mwisho ni kukata tamaa, lakini kumbuka
mpendwa, “Injili ni habari njema,” yaani - KATIKA KRISTO YESU, MUNGU
AMETUPATANISHA NAYE, YAANI AMETUPATIA TOBA, AMETUSAMEHE KABISA
DHAMBI ZETU NA KUIONDOA HATIA YETU, AMETUHESABIA HAKI NA KUTUPATIA
UZIMA WA MILELE (soma Yohana 3:16-17; 2 Kor. 5:18-19). Katika Kristo Yesu mbingu zimetoa
vyote na kutupatia vyote tunavyohitaji, hakuna upungufu (soma 2 Petro 1:3-4). Tusipoamini na
kuupokea ukweli huu, kamwe hatutakuwa na amani ya Kristo mioyoni (soma Yohana 14:27; Mathayo
11:28-30. Tukiupokea ukweli huu ndipo tutamtumikia Mungu kwa furaha, kwani tunafurahia
wokovu wetu. Na kwa vile tunapomwamini yesu, ni kuwa anaingia ndani yetu nasi ndani yake, basi
matendo hayo mema hayawi yetu sisi, bali ya Kristo aliyemo ndani yetu, ndipo sifa zote na utukufu
vitamrudia Mungu, naye atatukuzwa (soma Mathayo 5:16; Yohana 15:1-8). KUMBUKA, KUSUDI
Comments
Post a Comment