MFUNDISHE MTOTO KUOMBA KWA MUNGU

 


Ni muhimu kuwafundisha watoto kuomba pale tu wanapoweza kuongea. Huu ni wakati mwafaka kwa wewe mzazi kumfundisha mwanao kuongea na Mungu wake. Wakati huu unafaa sana maana ukisubiri awe mkubwa ndio umfundishe kuomba itakuwa vigumu sana kumwelewesha, anza mapema kumjengea msingi imara wa maombi.
Mtoto anatakiwa afundishwe kumshukuru Mungu kwa mambo mbalimbali ya maisha yake kama vile,afya, wazazi, , chakula, nguo na mengineyo mfano  kumwomba Mungu pale anapopata hofu, huzuni au kuumizwa. Ni vizuri pia ajifunze kuwaombea wadogo na wakubwa wake, walimu wake, marafiki zake na majirani pia. Hii itamjengea pia upendo kwa watu ambao anawaombea. Mweleze kuwa Mungu anampenda na anasikia maombi yake na anapenda kuzungumza naye.
Wazazi wanatakiwa kuomba na watoto  wakati wa Kula, akiamka asubuhi, usiku wakati wa kulala, anapoondoka kwenda shule na pale unapomuombea mtu mwenye mahitaji umfundishe kumshukuru Mungu pale maombi yake yanapojibiwa.

Comments

Popular posts from this blog

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

Ufanye Nini Unapoumizwa Moyo Na Watu Wako Wa Karibu/ Jinsi Ya Kupokea Uponyaji kwa Moyo Ulioumizwa