Miongozo Ya Kuishi Kwa Kufuata Biblia Na Zile Amri Kumi

 Kuziangalia kwa kifupi tu hizo Amri Kumi kutatusaidia kuelewa kwa nini hizo pamoja na Biblia hujenga msingi muhimu sana wa maisha yaliyo manyofu.

Amri hizo kwa kawaida huangukia katika sehemu kuu mbili. Zile nne za kwanza hufafanua uhusiano wetu na Mungu, na zile sita za mwisho hufafanua uhusiano wetu na watu wengine. Zinapatikana katika Kutoka 20:3-17.
Amri mbili za kwanza zinaelezea uhusiano wetu na Mungu pamoja na ibada yake.
I. "Usiwe na Miungu mingine ila Mimi".
II. "Usijifanyie sanamu ya kuchonga. Usizisujudie wala kuzitumikia…"

Amri ile ya 3 na ya 4 hueleza kwa juu juu tu uhusiano wetu na jina la Mungu na siku yake takatifu.
III. "Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako…"
IV. "Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako…"
Amri ya 5 na ya 7 inaimarisha vifungo vya familia.
V. "Waheshimu baba yako na mama yako…."
VI. "Usizini."
Amri ya 6, 8, 9 na 10 hutulinda sisi katika uhusiano wetu kijamii.
VII. Usiue."
VIII. "Usiibe."
IX. "Usimshuhudie jirani yako uongo."
X. "Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako….. wala chochote alicho nacho jirani yako."

Amri hizo kumi zinaweka mipaka ya uhusiano wetu kwa Mungu na kwa watu wengine. Hizo ni nguzo za kutuongoza katika mtindo wa maisha yetu ya Kikristo.

Comments

Popular posts from this blog

VINYWA VYA MOYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-2

LINDA SAANA MOYO WAKO KULIKO VYOTE ULINDAVYO: JINSI YA KULINDA MOYO WAKO-I

HAKI ZA WATOTO