SABABU ZA KUWAFUNDISHA WATOTO NENO LA MUNGU
(a) Watoto wanatakiwa wafahamu neno la Mungu na Mungu mwenyewe wakiwa wadogo
(b) Watoto wanatakiwa kuwezeshwa kumtii Yesu Kristo na neno lake
(c) Watoto wanatakiwa wajue kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli
(d) Watoto wanaomjua Kristo wanaweza kubadili Taifa/dunia ya kesho
(e) Watoto wanatayarishwa wawe watoto hai na kuwa viongozi wa kesho wanaongoza Kanisa katika njia sahihi
(f) Wawe viongozi wa kesho wanaongoza Taifa katika njia sahihi na hofu ya Mungu
Wazazi wetu wana hamu kubwa sana ya kuona watoto wao wanabarikiwa na kukua katika misingi ya Neno la Bwana. Ni wajibu wa mzazi Mkristo kuwafundisha watoto wakiwa bado na umri mdogo na hata atakapokuwa hataacha njia ya BWANA. Haya yote ni kwa ajili ya kutimiza maagizo ya Yesu ya aliyosema
Ni wajibu wetu kuwafundisha watoto namna Mungu anavyofanya kazi kwenye maisha ya watu wengine, ili waweze kujifunza na kuona kweli Mungu anaweza kubadilisha maisha ya watu na inawezekana kabisa kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Pia, tuwatie moyo katika maisha yao ya kiroho kila siku ili waweze kusonga mbele katika maisha yao.

Comments
Post a Comment